Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
2
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:
3
wazao wa Paroshi 2,172
4
wazao wa Shefatia 372
5
wazao wa Ara 775
6
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812
7
wazao wa Elamu 1,254
8
wazao wa Zatu 945
9
wazao wa Zakai 760
10
wazao wa Bani 642
11
wazao wa Bebai 623
12
wazao wa Azgadi 1,222
13
wazao wa Adonikamu 666
14
wazao wa Bigwai 2,056
15
wazao wa Adini 454
16
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
17
wazao wa Besai 323
18
wazao wa Yora 112
19
wazao wa Hashumu 223
20
wazao wa Gibari 95
21
watu wa Bethlehemu 123
22
watu wa Netofa 56
23
watu wa Anathothi 128
24
watu wa Azmawethi 42
25
wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
26
wazao wa Rama na Geba 621
27
watu wa Mikmashi 122
28
watu wa Betheli na Ai 223
29
wazao wa Nebo 52
30
wazao wa Magbishi 156
31
wazao wa Elamu ile ingine 1,254
32
wazao wa Harimu 320
33
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725
34
wazao wa Yeriko 345
35
wazao wa Senaa 3,630
36
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
37
wazao wa Imeri 1,052
38
wazao wa Pashuri 1,247
39
wazao wa Harimu 1,017
40
Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74
41
Waimbaji: wazao wa Asafu 128
42
Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139
43
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
44
wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,
45
wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,
46
wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,
47
wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,
48
wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,
49
wazao wa Uza, Pasea, Besai,
50
wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,
51
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
52
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
53
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
54
wazao wa Nesia na Hatifa.
55
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,
56
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
57
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.
58
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
59
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
60
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652
61
Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
62
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
63
Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
64
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
65
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.
66
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,
67
ngamia 435 na punda 6,720.
68
Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.
69
Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.
70
Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.