Psa 13

? AI
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpaka lini, Ee Bwana? Je, utanisahau milele? Utanificha uso wako mpaka lini?
2
Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda mpaka lini?
3
Nitazame, unijibu, Ee Bwana Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4
Adui yangu atasema, “Nimemshinda,” nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
5
Lakini ninategemea upendo wako usiokoma; moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6
Nitamwimbia Bwana, kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.
Global Bible Tools - Collaborative Bible translation platform