1 לַמְנַצֵּ֬חַ Kwa–kiongozi-wa-kwaya לִבְנֵי־ la–wana-wa קֹ֬רַח Kora מַשְׂכִּֽיל׃ maskili אֱלֹהִ֤ים ׀ Mungu בְּאָזְנֵ֬ינוּ kwa–masikio-yetu שָׁמַ֗עְנוּ tumesikia אֲבוֹתֵ֥ינוּ baba-zetu סִפְּרוּ־ wametusimulia לָ֑נוּ kwetu פֹּ֥עַל kazi פָּעַ֥לְתָּ ulifanya בִֽ֝ימֵיהֶ֗ם katika–siku-zao בִּ֣ימֵי katika–siku-za קֶֽדֶם׃ zamani
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametueleza yale uliyotenda katika siku zao, siku za kale.
2 אַתָּ֤ה ׀ Wewe יָדְךָ֡ mkono-wako גּוֹיִ֣ם mataifa ה֭וֹרַשְׁתָּ uliwafukuza וַתִּטָּעֵ֑ם na–ukawapanda תָּרַ֥ע uliwateswa לְ֝אֻמִּ֗ים watu וַֽתְּשַׁלְּחֵֽם׃ na–ukawasambaza
Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa na ukawapanda baba zetu, uliangamiza mataifa na kuwastawisha baba zetu.
3 כִּ֤י Kwa-kuwa לֹ֪א si בְחַרְבָּ֡ם kwa–upanga-wao יָ֥רְשׁוּ waliirithi אָ֗רֶץ nchi וּזְרוֹעָם֮ na–mkono-wao לֹא־ haukuwaokoa הוֹשִׁ֪יעָ֫ה kuwaokoa לָּ֥מוֹ kwao כִּֽי־ bali יְמִֽינְךָ֣ mkono-wako-wa-kuume וּ֭זְרוֹעֲךָ na–mkono-wako וְא֥וֹר na–nuru-ya פָּנֶ֗יךָ uso-wako כִּ֣י kwa-kuwa רְצִיתָֽם׃ uliwapenda
Sio kwa upanga wao waliipata nchi, wala si mkono wao uliwapatia ushindi; ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwapenda.
4 אַתָּה־ Wewe ה֣וּא yeye מַלְכִּ֣י Mfalme-wangu אֱלֹהִ֑ים Mungu צַ֝וֵּ֗ה amuru יְשׁוּע֥וֹת wokovu-za יַעֲקֹֽב׃ Yakobo
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
5 בְּ֭ךָ Kwako צָרֵ֣ינוּ adui-zetu נְנַגֵּ֑חַ tutawasukuma בְּ֝שִׁמְךָ֗ kwa–jina-lako נָב֥וּס tutawakanyaga קָמֵֽינוּ׃ wanaosimama-dhidi-yetu
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
6 כִּ֤י Kwa-kuwa לֹ֣א si בְקַשְׁתִּ֣י upinde-wangu אֶבְטָ֑ח nitaamini וְ֝חַרְבִּ֗י na–upanga-wangu לֹ֣א hauta תוֹשִׁיעֵֽנִי׃ kuniokoa
Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi;
7 כִּ֣י Kwa-kuwa ה֭וֹשַׁעְתָּנוּ umetuokoa מִצָּרֵ֑ינוּ kutoka–adui-zetu וּמְשַׂנְאֵ֥ינוּ na–wanaotuchukia הֱבִישֽׁוֹתָ׃ umewaaibiisha
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.
8 בֵּֽ֭אלֹהִים Kwa–Mungu הִלַּלְ֣נוּ tumejimuimba כָל־ siku-nzima הַיּ֑וֹם siku וְשִׁמְךָ֓ ׀ na–jina-lako לְעוֹלָ֖ם milele נוֹדֶ֣ה tutashukuru סֶֽלָה׃ Sela
Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele.
9 אַף־ Lakini זָ֭נַחְתָּ umetukataa וַתַּכְלִימֵ֑נוּ na–umetufedhehesha וְלֹא־ na–hutoki תֵ֝צֵ֗א utoke בְּצִבְאוֹתֵֽינוּ׃ pamoja-na–majeshi-yetu
Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.
10 תְּשִׁיבֵ֣נוּ Unaturudisha אָ֭חוֹר nyuma מִנִּי־ kutoka–kwa צָ֑ר adui וּ֝מְשַׂנְאֵ֗ינוּ na–wanaotuchukia שָׁ֣סוּ wametunyang'anya לָֽמוֹ׃ kwao
Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara.
11 תִּ֭תְּנֵנוּ Umetutoa כְּצֹ֣אן kama–kondoo מַאֲכָ֑ל chakula וּ֝בַגּוֹיִ֗ם na–miongoni-mwa–mataifa זֵרִיתָֽנוּ׃ umetutawanya
Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa.
12 תִּמְכֹּֽר־ Unawauza עַמְּךָ֥ watu-wako בְלֹא־ bila ה֑וֹן utajiri וְלֹ֥א־ na–huku רִ֝בִּ֗יתָ kujipatia-faida בִּמְחִירֵיהֶֽם׃ kwa–bei-yao
Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.
13 תְּשִׂימֵ֣נוּ Umetufanya חֶ֭רְפָּה shutuma לִשְׁכֵנֵ֑ינוּ kwa–jirani-zetu לַ֥עַג dhihaka וָ֝קֶ֗לֶס na–mzaha לִסְבִיבוֹתֵֽינוּ׃ kwa–wanaotuzunguka
Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.
14 תְּשִׂימֵ֣נוּ Umetufanya מָ֭שָׁל mithali בַּגּוֹיִ֑ם miongoni-mwa–mataifa מְנֽוֹד־ kutikisa רֹ֝֗אשׁ kichwa בַּל־ miongoni-mwa אֻמִּֽים׃ watu
Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao.
15 כָּל־ Siku-nzima הַ֭יּוֹם siku כְּלִמָּתִ֣י fedheha-yangu נֶגְדִּ֑י mbele-yangu וּבֹ֖שֶׁת na–aibu-ya פָּנַ֣י uso-wangu כִּסָּֽתְנִי׃ imenifunika
Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele,
16 מִ֭קּוֹל Kwa-sababu-ya–sauti-ya מְחָרֵ֣ף anayeshutumu וּמְגַדֵּ֑ף na–anayetukana מִפְּנֵ֥י kwa-sababu-ya א֝וֹיֵ֗ב adui וּמִתְנַקֵּֽם׃ na–mjilipiza-kisasi
kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.
17 כָּל־ Haya-yote זֹ֣את hii בָּ֭אַתְנוּ yametujia וְלֹ֣א na–hatukukusahau שְׁכַחֲנ֑וּךָ kukusahau וְלֹֽא־ na–hatu שִׁ֝קַּ֗רְנוּ kudanganya בִּבְרִיתֶֽךָ׃ katika–agano-lako
Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.
18 לֹא־ Haukurudi נָס֣וֹג kurudi אָח֣וֹר nyuma לִבֵּ֑נוּ moyo-wetu וַתֵּ֥ט na–hazikugeuka אֲשֻׁרֵ֗ינוּ hatua-zetu מִנִּ֥י kutoka אָרְחֶֽךָ׃ njia-yako
Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
19 כִּ֣י Ingawa דִ֭כִּיתָנוּ ulituponda בִּמְק֣וֹם mahali-pa תַּנִּ֑ים mbweha וַתְּכַ֖ס na–ukafunika עָלֵ֣ינוּ juu-yetu בְצַלְמָֽוֶת׃ kwa–kivuli-cha-mauti
Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.
20 אִם־ Kama שָׁ֭כַחְנוּ tulisahau שֵׁ֣ם jina-la אֱלֹהֵ֑ינוּ Mungu-wetu וַנִּפְרֹ֥שׂ na–tukaeneza כַּ֝פֵּ֗ינוּ mikono-yetu לְאֵ֣ל kwa–mungu זָֽר׃ mgeni
Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
21 הֲלֹ֣א Je-si אֱ֭לֹהִים Mungu יַֽחֲקָר־ atachunguza זֹ֑את hii כִּֽי־ kwa-kuwa ה֥וּא yeye יֹ֝דֵ֗עַ anajua תַּעֲלֻמ֥וֹת siri-za לֵֽב׃ moyo
je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?
22 כִּֽי־ Hakika עָ֭לֶיךָ kwa-ajili-yako הֹרַ֣גְנוּ tunauawa כָל־ siku-nzima הַיּ֑וֹם siku נֶ֝חְשַׁ֗בְנוּ tunahesabiwa כְּצֹ֣אן kama–kondoo-wa טִבְחָֽה׃ machinjio
Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
23 ע֤וּרָה ׀ Amka לָ֖מָּה Kwa-nini תִישַׁ֥ן ׀ unalala אֲדֹנָ֑י Bwana הָ֝קִ֗יצָה Amka אַל־ usi תִּזְנַ֥ח kutupilia-mbali לָנֶֽצַח׃ milele
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
24 לָֽמָּה־ Kwa-nini פָנֶ֥יךָ uso-wako תַסְתִּ֑יר unaficha תִּשְׁכַּ֖ח unasahau עָנְיֵ֣נוּ mateso-yetu וְֽלַחֲצֵֽנוּ׃ na–uonevu-wetu
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
25 כִּ֤י Kwa-kuwa שָׁ֣חָה imeinamishwa לֶעָפָ֣ר mavumbini נַפְשֵׁ֑נוּ nafsi-yetu דָּבְקָ֖ה imeshikamana לָאָ֣רֶץ ardhini בִּטְנֵֽנוּ׃ tumbo-letu
Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.
26 ק֭וּמָֽה Simama עֶזְרָ֣תָה utusaidie לָּ֑נוּ kwetu וּ֝פְדֵ֗נוּ na–utukomboe לְמַ֣עַן kwa-sababu-ya חַסְדֶּֽךָ׃ upendo-wako-wa-agano
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.