Psa 149

? AI
1
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Global Bible Tools - Collaborative Bible translation platform