1 דִּבְרֵי֙ Maneno–ya קֹהֶ֣לֶת Mhubiri בֶּן־ mwana–wa דָּוִ֔ד Daudi מֶ֖לֶךְ mfalme בִּירוּשָׁלִָֽם׃ katika–Yerusalemu
Maneno ya Mhubiri, mwana wa Daudi, mfalme huko Yerusalemu:
2 הֲבֵ֤ל Ubatili הֲבָלִים֙ wa–ubatili אָמַ֣ר alisema קֹהֶ֔לֶת Mhubiri הֲבֵ֥ל ubatili הֲבָלִ֖ים wa–ubatili הַכֹּ֥ל yote הָֽבֶל׃ ni–ubatili
“Ubatili mtupu! Ubatili mtupu!” Mhubiri anasema. “Ubatili mtupu! Kila kitu ni ubatili.”
3 מַה־ Nini יִּתְר֖וֹן faida לָֽאָדָ֑ם kwa–mwanadamu בְּכָל־ katika–kila עֲמָל֔וֹ kazi–yake שֶֽׁיַּעֲמֹ֖ל anayofanya תַּ֥חַת chini–ya הַשָּֽׁמֶשׁ׃ jua
Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote anayotaabikia chini ya jua?
4 דּ֤וֹר Kizazi הֹלֵךְ֙ kinaenda וְד֣וֹר na–kizazi בָּ֔א kinakuja וְהָאָ֖רֶץ lakini–dunia לְעוֹלָ֥ם milele עֹמָֽדֶת׃ inabaki
Vizazi huja na vizazi hupita, lakini dunia inadumu milele.
5 וְזָרַ֥ח Na–huchomoza הַשֶּׁ֖מֶשׁ jua וּבָ֣א na–hutua הַשָּׁ֑מֶשׁ jua וְאֶ֨ל־ na–kwenye מְקוֹמ֔וֹ mahali–pake שׁוֹאֵ֛ף hukimbilia זוֹרֵ֥חַֽ kuchomoza ה֖וּא yeye שָֽׁם׃ huko
Jua huchomoza na jua huzama, nalo huharakisha kurudi mawioni.
6 הוֹלֵךְ֙ Huenda אֶל־ kuelekea דָּר֔וֹם kusini וְסוֹבֵ֖ב na–huzunguka אֶל־ kuelekea צָפ֑וֹן kaskazini סוֹבֵ֤ב ׀ kuzunguka סֹבֵב֙ kuzunguka הוֹלֵ֣ךְ huenda הָר֔וּחַ upepo וְעַל־ na–juu–ya סְבִיבֹתָ֖יו mizunguko–yake שָׁ֥ב hurudi הָרֽוּחַ׃ upepo
Upepo huvuma kuelekea kusini na kugeukia kaskazini, hurudia mzunguko huo huo, daima ukirudia njia yake.
7 כָּל־ Yote הַנְּחָלִים֙ mito הֹלְכִ֣ים inaenda אֶל־ kuelekea הַיָּ֔ם bahari וְהַיָּ֖ם lakini–bahari אֵינֶ֣נּוּ haijazidi מָלֵ֑א kujaa אֶל־ kuelekea מְק֗וֹם mahali שֶׁ֤הַנְּחָלִים֙ ambako–mito הֹֽלְכִ֔ים inaenda שָׁ֛ם huko הֵ֥ם wao שָׁבִ֖ים hurudi לָלָֽכֶת׃ kwenda
Mito yote hutiririka baharini, hata hivyo bahari kamwe haijai. Mahali mito inapotoka, huko hurudi tena.
8 כָּל־ Vitu–vyote הַדְּבָרִ֣ים mambo יְגֵעִ֔ים yanachosha לֹא־ hawezi יוּכַ֥ל mtu אִ֖ישׁ mtu לְדַבֵּ֑ר kusema לֹא־ haishbii תִשְׂבַּ֥ע jicho עַ֙יִן֙ jicho לִרְא֔וֹת kuona וְלֹא־ wala–haijazi תִמָּלֵ֥א sikio אֹ֖זֶן sikio מִשְּׁמֹֽעַ׃ kusikia
Vitu vyote vinachosha, zaidi kuliko mtu anavyoweza kusema. Jicho kamwe halitosheki kutazama, wala sikio halishibi kusikia.
9 מַה־ Nini שֶּֽׁהָיָה֙ kilichokuwa ה֣וּא ndicho שֶׁיִּהְיֶ֔ה kitakachokuwa וּמַה־ na–nini שֶׁנַּֽעֲשָׂ֔ה kilichofanywa ה֖וּא ndicho שֶׁיֵּעָשֶׂ֑ה kitakachofanywa וְאֵ֥ין na–hakuna כָּל־ chochote חָדָ֖שׁ kipya תַּ֥חַת chini–ya הַשָּֽׁמֶשׁ׃ jua
Kile kilichokuwepo kitakuwepo tena, kile kilichofanyika kitafanyika tena, hakuna kilicho kipya chini ya jua.
10 יֵ֥שׁ Kuna דָּבָ֛ר jambo שֶׁיֹּאמַ֥ר ambalo–mtu–anasema רְאֵה־ Tazama זֶ֖ה hili חָדָ֣שׁ ni–kipya ה֑וּא hilo כְּבָר֙ tayari הָיָ֣ה lilikuwa לְעֹֽלָמִ֔ים kwa–vizazi אֲשֶׁ֥ר ambavyo הָיָ֖ה vilikuwa מִלְּפָנֵֽנוּ׃ kabla–yetu
Kuna kitu chochote ambacho mtu anaweza kusema, “Tazama! Kitu hiki ni kipya”? Kilikuwepo tangu zamani za kale, kilikuwepo kabla ya wakati wetu.
11 אֵ֥ין Hakuna זִכְר֖וֹן kumbukumbu לָרִאשֹׁנִ֑ים ya–wa–kwanza וְגַ֨ם na–pia לָאַחֲרֹנִ֜ים wa–baadaye שֶׁיִּהְי֗וּ watakaokuwa לֹֽא־ hawatakuwa יִהְיֶ֤ה na לָהֶם֙ kwao זִכָּר֔וֹן kumbukumbu עִ֥ם pamoja–na שֶׁיִּהְי֖וּ watakaokuwa לָאַחֲרֹנָֽה׃ baadaye פ —
Hakuna kumbukumbu ya watu wa zamani, hata na wale ambao hawajaja bado hawatakumbukwa na wale watakaofuata baadaye.
12 אֲנִ֣י Mimi קֹהֶ֗לֶת Mhubiri הָיִ֥יתִי nilikuwa מֶ֛לֶךְ mfalme עַל־ juu–ya יִשְׂרָאֵ֖ל Israeli בִּירוּשָׁלִָֽם׃ katika–Yerusalemu
Mimi, Mhubiri, nilikuwa mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.
13 וְנָתַ֣תִּי Na–nikaweka אֶת־ — לִבִּ֗י moyo–wangu לִדְר֤וֹשׁ kutafuta וְלָתוּר֙ na–kuchunguza בַּֽחָכְמָ֔ה kwa–hekima עַ֛ל kuhusu כָּל־ yote אֲשֶׁ֥ר yanayofanywa נַעֲשָׂ֖ה yanayofanywa תַּ֣חַת chini–ya הַשָּׁמָ֑יִם mbingu ה֣וּא ׀ huu עִנְיַ֣ן kazi רָ֗ע ngumu נָתַ֧ן aliyotoa אֱלֹהִ֛ים Mungu לִבְנֵ֥י kwa–wana–wa הָאָדָ֖ם wanadamu לַעֲנ֥וֹת kujishughulisha בּֽוֹ׃ nayo
Nilitumia muda wangu wote kujifunza na kuvumbua kwa hekima yote yanayofanyika chini ya mbingu. Jinsi gani Mungu ameweka mzigo mzito juu ya wanadamu!
14 רָאִ֙יתִי֙ Nimeona אֶת־ — כָּל־ yote הַֽמַּעֲשִׂ֔ים matendo שֶֽׁנַּעֲשׂ֖וּ yanayofanywa תַּ֣חַת chini–ya הַשָּׁ֑מֶשׁ jua וְהִנֵּ֥ה na–tazama הַכֹּ֛ל yote הֶ֖בֶל ni–ubatili וּרְע֥וּת na–kufuata רֽוּחַ׃ upepo
Nimeshaona mambo yote yanayotendeka chini ya jua, hayo yote ni ubatili, hii ni kukimbiza upepo.
15 מְעֻוָּ֖ת Kilichopotoka לֹא־ hakiwezi יוּכַ֣ל kunyooshwa לִתְקֹ֑ן kunyooshwa וְחֶסְר֖וֹן na–upungufu לֹא־ hauwezi יוּכַ֥ל kuhesabiwa לְהִמָּנֽוֹת׃ kuhesabiwa
Kilichopindika hakiwezi kunyooshwa, kile ambacho hakipo haiwezekani kukihesabu.
16 דִּבַּ֨רְתִּי Niliongea אֲנִ֤י mimi עִם־ na לִבִּי֙ moyo–wangu לֵאמֹ֔ר nikisema אֲנִ֗י mimi הִנֵּ֨ה tazama הִגְדַּ֤לְתִּי nimekuwa–mkubwa וְהוֹסַ֙פְתִּי֙ na–nimeongeza חָכְמָ֔ה hekima עַ֛ל kuliko כָּל־ wote אֲשֶׁר־ waliokuwa הָיָ֥ה walikuwa לְפָנַ֖י kabla–yangu עַל־ juu–ya יְרוּשָׁלִָ֑ם Yerusalemu וְלִבִּ֛י na–moyo–wangu רָאָ֥ה umeona הַרְבֵּ֖ה mengi חָכְמָ֥ה hekima וָדָֽעַת׃ na–maarifa
Niliwaza mwenyewe, “Tazama, nimekua na kuongezeka katika hekima kuliko yeyote aliyewahi kutawala Yerusalemu kabla yangu. Nimekuwa na uzoefu mkubwa wa hekima na maarifa.”
17 וָאֶתְּנָ֤ה Na–nikaweka לִבִּי֙ moyo–wangu לָדַ֣עַת kujua חָכְמָ֔ה hekima וְדַ֥עַת na–kujua הוֹלֵל֖וֹת wazimu וְשִׂכְל֑וּת na–upumbavu יָדַ֕עְתִּי nilijua שֶׁגַּם־ kwamba–hii–pia זֶ֥ה hii ה֖וּא ni רַעְי֥וֹן kufuata רֽוּחַ׃ upepo
Ndipo nilipojitahidi kufahamu kutofautisha hekima, wazimu na upumbavu, lakini nikatambua hata hili nalo ni kukimbiza upepo.
18 כִּ֛י Kwa–sababu בְּרֹ֥ב katika–wingi–wa חָכְמָ֖ה hekima רָב־ wingi–wa כָּ֑עַס huzuni וְיוֹסִ֥יף na–anayeongeza דַּ֖עַת maarifa יוֹסִ֥יף huongeza מַכְאֽוֹב׃ maumivu
Kwa kuwa hekima nyingi huleta huzuni kubwa; maarifa yanapoongezeka, masikitiko yanaongezeka.