Psa 114

? AI
1
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Global Bible Tools - Collaborative Bible translation platform