Psa 111

? AI
1
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
Global Bible Tools - Collaborative Bible translation platform